Saturday, June 16, 2012


Saturday, June 9, 2012

TENGA AAGIZA UCHUNGUZI UFANYIKE SAKATA LA YONDANI KUONDOKA KAMBI YA STARS KWENDA KUSAINI MKATABA YANGA

Saturday, June 9, 2012

 

 
 


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KLABU ya soka ya Simba imepokea kwa furaha taarifa kwamba Rais wa Shirikisho la Mpira was Miguu Tanzania (TFF), Leodger Chila Tenga, ameagiza kufanyika kwa uchunguzi kuhusiana na namna mchezaji wa Simba na Taifa Stars, Kelvin Patrick Yondani, alivyoondoka kambini usiku wa kuamkia Juni 7 mwaka huu.
Katika barua ambayo Tenga ameiandikia Simba, ameahidi kwamba uchunguzi utafanyika katika maeneo makuu mawili. Mosi, iwapo ni kweli Yondani aliondoka kambini usiku, pili iwapo aliondoka kwa ruhusa maalumu au alitoroka. 
Tenga ameahidi kwamba kama ikibainika kwamba aliondoka bila ruhusa, basi hatua zitachukuliwa kwa wote waliohusika chini ya taratibu za maadili kwa wachezaji  (Players Code of Conduct).
Kutokana na kauli hiyo ya Tenga, uongozi wa Simba umeamua sasa kwamba hautozungumza lolote kuhusiana na masuala ya Yondani. Tayari timu imewasilisha vielelezo vyake TFF na kote kwingine ambako suala hilo linaweza kufika. Kilichobaki sasa ni kusubiri vyombo husika vifanye kazi yake.
Simba SC inapenda kuchukua nafasi hii kuwaomba wapenzi na wanachama wake kutulia na kutobabaishwa na taarifa za wachezaji wake kusajiliwa na timu nyingine. 
Kwa sasa Simba inaendelea na mikakati yake ya usajili unaokidhi vigezo vya kimataifa ambao ulisababisha msimu uliopita itwae ubingwa wa Tanzania na kuifunga YANGA goli 5-0 !
Simba si timu ya maneno mengi kwenye usajili bali ni vitendo. 
Tunaomba wanachama wetu watulie na mara ifikapo tareje 15 Juni mwaka huu, mbivu na mbichi zote zitajulikana. Siku hiyo, Simba itatangaza wachezaji wake wote iliyowasajili na iliyowaacha. 
Simba ndiyo mabingwa wa Tanzania na washabiki wake wanatakiwa kutembea vifua mbele popote pale walipo na wasichanganywe na taarifa za pembeni. 
Uongozi wa Simba uko makini na unafanya kazi zake kisayansi.

Imetolewa na 

Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC

KUELEKEA MCHEZO WA GAMBIA KESHO-POULSEN ALIA NA TFF


TIMU ya soka ya Taifa ‘Kili Taifa Stars’ kesho inashuka katika dimba la Taifa jijini Dar es Salam kukwaana na Gambia ‘The Scorpions’ katika mchezo wa mchujo wa kuwania kucheza fainali za kombe la dunia 2014 zitakazopigwa nchini Brazil. 
Akizungumza na waandishi wa habari,kocha mkuu wa Stars,  Mdenmark Kim Poulsen  alisema kikosi kikosi chake kipo katika hali nzuri ya kimchezo ambao anaamini utakuwa na upinzani mkubwa.
 Hata hivyo, Poulsen alisikitishwa TFF kutompatia  DVD za mechi za Gambia ili iweze kuwasaidia katika maandalizi ya mchezo wa kesho na kuongeza kuwa hii ni mara ya pili kushindwa kupatiwa DVD hizo ambapo awali ilikuwa katika mchezo dhidi ya Ivory Coast ambapo Stars ililala mabao 2-0.
 “Pamoja na kuzikosa DVD hizo nimekiandaa kikosi changu kukabiliana na Gambia ambapo naamini watatumia vizuri uwanja wa nyumbani kwa kushinda mabao mengi,”alisema.
 Poulsen aliongeza kuwa wachezaji wake wapo katika hali nzuri isipokuwa Nurdin bakari, huku kiungo mshambuliaji Haruna Moshi ‘Boban’ aliyekuwa majeruhi hali yake ikiimarika na huenda leo akampanga dimbani.
 Hata hivyo mchezo wa kesho  unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa na hasa ikizingatiwa kila timu inahitaji ushindi ambapo Gambia ilitoka sare ya bao 1-1  Morocco na Morocco katika mchezo wao ulipigwa nyumbani wiki iliyopita. 
Kocha wa Gambia, Mtaliano Luciano Machini akizungumza jana katika mazoezi yao kwenye uwanja wa Karume, alisema  itakuwa ngumu kwa sababu wapinzani wao ni wazuri na wana kasi uwanjani.
 Mchezo huo utakapigwa kuanzia saa 10.00 jioni na kuchezeshwa na waamuzi kutoka nchini Zimbabwe,  Ruzive Ruzive akisaidiwa na Salani Ncube na Edger Rumeck ambapo tiketi zimeanza kuuzwa leo  katika vituo mbalimbali huku kesho  zoezi hilo litahamia uwanja wa Taifa kuazia saa 6 mchana.
 Viingilio katika mchezo huo ni  sh.3,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, huku sh.5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, wakati VIP C watalipa sh. 10,000 ,  VIP B watalipa sh. 20,000 na watakaokaa VIP A watalipa  sh. 30,000.

AZAM FC KUANZA KUJINOA J'3

MABINGWA wa kombe la Mapinduzi Azam Fc jumatatu ya keshokutwa inatarajiwa kuanza kujinoa kwa ajili ya michuano ya kombe la Kagame itakayoanza kutimua vumbi jijini Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi huu.
Msemaji wa msaidizi wa Azam Fc Jaffer Idd Maganga amesema kwamba wachezaji wote wanatakiwa kuripoti kamni siku hiyo tayari kuanza mazoezi yao.
Azam Fc inayonolewa na Muingereza Stewart Hall, pia ni wa shindi wa pili wa ligi kuu soka Tanzabnia Bara

SAMATTA HUYOOOOO MAN CITY

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mbwana Samatta, huenda akajiunga na mabingwa wa Ligi Kuu England, Man City.
Habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam zinaeleza kwamba nyota huyo aliyeibukia Simba Sc kwa sasa yupo katika mazungumzo na mawakala wa Ulaya ili aweze kwenda kufanya majaribio Man City na hatimaye kujiunga nayo iwapo atafuzu majaribio yake.
Imeelezwa kuwa, mawakala hao wameshawasili Kinshasha, DRC na kuanza mazungumzo na uongozi wa klabu ya TP Mazembe kuhusina na nyota huyo ambaye pia anakipiga katika timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars.
Samatta alijuiunga na TP Mazembe akitokea Simba kwa dau la dola 200,000.

JERRY TEGETE AIZODOA SIMBA SC


KLABU ya soka ya Yanga imewapiga tena bao la kisigino mahasimu wao wa jadi nchini Simba baada ya  kumuongezea mkataba wa miaka miwili nyota wake  Jerryson Tegete.
 Wakati ligi kuu soka Tanzania Bara ikielekea ukiongoni, Simba ambao ni mabingwa wa ligi hiyo walianza mpango wa kutaka kumsajili mchezaji huyo baada ya kuwepo taarifa kutoka Yanga kwamba haina mpango naye tena.
 Hata hivyo, baada ya tetesi za Simba kumuwania Tegete kuzagaa mtaani ndipo Yanga iliporudi nyuma na kuamua kumfunga mchezaji huyo ambaye mkataba wake ulikuwa unalizika mwezi huu hadi mwaka 2014.
 Mmoja ya wadau wa Yanga wanaohusika na usajili wa wachezaji katika klabu ya Yanga alisema jana kwamba wameamua kumbakiza kundini Tegete kutokana na umuhimu alionao katika kikosi hicho.
 “Napenda niwatoe shaka wanayanga kwamba kwa Tegete ataendelea kuvaa uzi wa njano na kijani kwa miaka miwili…wale walikuwa wakimuwania nawapa pole kwani ameshamwaga wino jangwani,”alisema.
 Tegete ambaye  msimu uliopita hakuweza kung’ara  alitua Yanga mwaka 2008, akitokea sekondari ya Makongo, ambapo kutokana na umahiri alionao kwa nyakati tofauti alipata kuichezea timu ya Taifa ‘Taifa Stars’.
 Yanga ambayo kwa sasa imeingia vita na Simba baada ya kumsainisha mkataba wa miaka miwili nyota wake Kelvin Yondan ‘Vidic’, pia imeshamsajili kipa wa Simba  Ally Mustafa  ‘Barthez’ ikionekana kama kulipa kisasi baada ya Simba kumsajili  Kiggi Makassy.

KHADIJA KOPA KUPAMBA MISS LAKE ZONE INTERCOLLEGE 2012


Malkia wa mipasho na mshindi wa tuzo za Tanzania Kili music Awards 2012 Khadija Kopa anategemewa kuwa kivuto kikubwa kwa kutoa burudani ya kipekee katika shindano la kumsaka mlimbwende wa MISS lAKE ZONE INTERCOLLEGES 2012 ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika mkoani Kagera katika mji wa Bukoba.
  Akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es salaam Mwandaaji wa shindano hilo Bw.Joseph Rwebangira amesema kuwa asilimia kubwa ya maandalizi yameshatimia,hata hivyo Rwebangira aliongezea kuwa mshereheshaji wa siku hiyo atakuwa mchekeshaji maarufu afrika mashariki na kati Mpoki wa the origina comedy.
   Miss Lake zone Intercolleges 2012 inayoandaliwa na kampuni ya Angles Real Entertainment ya jijini Dar es salaam chini ya Mkurugezi wake Joseph Rwebangira imejipanga vya kutosha kuleta mabadiliko ikiwa na lengo la kumfikisha mrembo wake katika ngazi ya fainali kitaifa.
   Shindano hilo litafanyika katika ukumbi wa Linuz Club uliopo Bukoba mjini siku ya jumamosi tarehe  23 juni ambapo mbali ya hayo kutakuwa na burudani za ngoma za asili na wasanii wa mkoa wa Kagera,pia kiingilio kitakuwa ni Tsh 10,000/= kawaida na V.I.P ni Tshs 15,000/=

YONDAN NUSURA ATIMULIWE STARS, TFF YAGOMA KUZUNGUMZIA SAKATA LAKE

BEKI wa kati wa timu ya Simba Kelvin Yondan nusura atimuliwe katika kambi ya timu ya Taifa baada ya kutoroka na kwenda kusaini mkataba na klabu ya Yanga.
Habari kutoka kambi ya Stars iliyopo hoteli ya Tansoma katikati ya jiji la Dar es Salaam zinaeleza kuwa kocha mkuu wa Stars Kim Poulsen alimuweka kiti moto nyota huyo baada ya kubaini kuwa hakuwepo kambini usiku wa juzi, lakini baada ya kujitetea ndipo alipoamua kumsamehe.
Uongozi wa Simba kupitia mwenyekiti wake Alhaj Ismail Aden Rage umesisirtiza kuwa Yondan ni mchezaji wake halali na kwamba Yanga wamebugi step kumsainisha mkataba mptya.
Kama hiyo haitoshi, Rage alisema wanatarajiwa kufikisha suala hilo kwa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) na lile la Kimataifa (FIFA) kwani hata mkataba wenyewe huo una utata katika baadhi ya vipengele, huku kiongozi aliyeshiriki kusimamia zoezi hilo si kiongozi halali wa Yanga.
Huku hayo yakiendelea, TFF kupitia kwa msemaji wake Boniface Wambura imeshindwa kuzungumzia juu ya sakata hilo na kuombwa lipewe nmuda kwanza ya kutafuta vielelezo kuhusina na mchezaji huyo ambaye amelamba kitita cha shilingi mil.30 kwa ajili ya kumwaga wino Yanga ambapo pia atakuwa akilambva mshahara wa sh.800,000 kwa mwezi.
vinginevyo kwa kuthubutu na kujiamini, sifa ambazo mimi ninazo.

Naamini kwa pamoja tutajenga Yanga Bora na Yanga Imara.
YONO STANLEY KEVELA

 

STORY OF THE WEEK



Are you a ware that  mood swings and idiosyncratic behaviors of our workmates, friends and brothers may be a sign of mental disorder? George Adriano writes

When I set my eyes on her, she looked away! Jolie is a beautiful young girl of 21 years old. She is leading a single life after dropping out of school at form five. She is not employed and stays  with her grandparents at Gongo la Mboto.
I failed to restrict myself and said, “Talk to me baby!” She was shocked at my voice like someone from deep thoughts, but she kept quiet. “I am sorry” I said. She didn’t answer anything and instead walked away.
  I decided to inquire from the other girl who was standing next to me about this beautiful quiet girl. She was her elder Sister, Nashie. “Is she dumb?” I asked.  “No! She is my young sister, her name is Jolie” Nashie replied. “Is she mentally okay?” “Yes”  “So what is wrong? Did I offend her?” Mmh! Nashie was not sure but she told me a full story about Jolie.
Jolie was very okay until three years earlier when she insidiously started being very shy. She avoided walking together with other students and sometime covered her face with clothes. Later on she did so even to her close family members. 

After some months, she refused coming out of her room and she was looking at herself in a mirror complaining that she looked ugly with ‘a big nose’ and that other people will laugh at her. She ended up breaking the mirror. She was very irritable when forced to come out of her room.

Later she also developed insomnia. Sleeping at midnight and getting up very early at around 4.00 a.m and remaining a wake on the bed. Strange enough, she even spent most of the day time in the bedroom not actually sleeping but engrossed in her own thoughts. She also lost appetite, ate with difficulties ending up into food wastage as noted by her relatives.
It took her a year, and then she completely refused to go to school. She lost interest in various daily activities like cooking, watching TV or fetching water claiming that all these were boring and life was not good.
Two years before, their father had died after being involved in a tragic road accident with a motorcycle, Jolie felt very sorrowful and  spent most of the days and nights thinking  about her father.
In the same year, something happened to Jolie, when she was fetching some water from a shallow well, a stone throw  distance from home at around 8:00 pm, a middle aged man abused her sexually (forcefully, he had unprotected sex with her). She narrated the story to her relatives, but no action was taken against the perpetrator, she felt very bad but she was unable to do anything. Consequently, she has been experiencing lower abdominal pains even when not in menses.
I told my friend who is a doctor, about Jolie, the girl whom I loved so much. This was his response;
Doctor: Does your friend Jolie have a big nose?
Me: Aah No! She has a small really cute nose, I admire it.
Doctor: Jolie might be suffering from mood disorders. Mood disorders involve the disabling of the emotions.  It is convincing that, Jolie has Major Depressive Disorder (MDD), which is one of the mood disorders. She may also have somatoform disorder as she thinks that she has a big nose. The doctor offered  me a cold yet insightful analyses of mental disorders which opened my understanding with regards to Jolie.
He explained that depression is an emotional state characterized by,
·         Sadness or loss of connection with the ordinary world
·         Feelings of worthlessness and guilt. You may not think that you are a valuable person which leads to having low self esteem.
·         Withdrawal from others. you isolate yourself.
·         Lack of sleep; You don’t fall asleep though you may need to sleep
·         Reduced or loss of appetite.
·         Lack of sexual desire. The victim may erect and perform but minus the usual testosterone triggered urge
·         You may attempt or think to commit suicide, arguing that it’s better to die rather than to live
·         Inability to concentrate which occurs nearly every day.
·         Depression impairs important normal functions (such as work or personal relationships).
·         Drugs, alcohol, or other substances do not cause them.
When these conditions persist for two weeks (14 days) or more, then it is a Major Depressive Disorder. A person loses interest in most of the things or activities she/he used to enjoy. It is mostly prevalent among people of above 25 years. The duration and the severity of the symptoms vary. The likely cause of the ailment depends on several factors: a manifestation of a previous mental illness to the individual and sometimes having a relative who has ever suffered from the same (genetics) poor social support, poor adherence to the medication .However, faith in God can help to deal with mental disorders whereby the patient surrenders to the divine providence. A good job or a healthy relationship which you enjoy can also immunize someone against them.
Me: My God! Is it a mental problem?
Doctor: Oh, yes. It’s a psychological condition but as you can see it may affect the social, economic and spiritual life of a person.
Me: I am finished. Okay, thank you, bye!
Doctor: Hey! Sit please! I have not finished. This condition is curable. There are several ways of helping your friend which will undoubtedly restore her former self and you will go on enjoying life with her
Medication is among the modalities of treating Major Depressive Disorder. The medical treatment is usually accompanied by Psychological, social and even spiritual therapy. It’s quite common for the symptoms to diminish and then appear again after a period of time.
Me: Huuu! What should I do?
Doctor: It’s better to take your friend to the mental health professionals; clinical psychologists, and a psychiatrist. It’s very important to adhere to the medication in terms of dosage and duration, and make follow up to the mental clinic. Consult your doctor for any adverse changes which Jolie may notice in the course of treatment.
Me: Okay, thank you very much. Bye
When I was just about to shut the door and walk out, the doctor reminded me  not to forget  testing for HIV/Aids both of us, and pregnancy test for Jolie.
Written by;
Mwitha Thomas
Computer science student at UDSM
Mob: +255 714689297

Thursday, June 7, 2012


TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA CHAMA CHA MAPINDUZI UTAKAOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA JANGWANI, SIKU YA JUMAMOSI, TAREHE 09-06-2012.


TANGAZO:
Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kimeandaa Mkutano Mkubwa wa Hadhara kwa wananchi wote, Siku ya Jumamosi, tarehe 09/06/2012, Katika Viwanja vya Jangwani Kuanzia saa 8 mchana.
Maudhui; “ Kutoa Msimamo Wake Juu ya Masuala Yanayogusa Mustakabali wa Taifa. Hivyo Chama Kitatumia Fursa hiyo Kuelezea Watanzania Juu ya Msimamo Wake Katika Mambo yafuatayo:
1. Hatma ya maisha ya Watanzania
· Ajira
· Miundo mbinu ya Barabara, Reli, Bandari Na Anga.
· Bei za bidhaa mbalimbali.
· Umeme
· Rasilimali za taifa
2. Msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya.
3. Vurugu za Zanzibar.
Katika Mkutano huo, Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali watakuwepo na kutoa ufafanuzi juu ya masuala hayo yaliyoainishwa kama msimamo wa Chama Cha Mapinduzi.
Chama Cha Mapinduzi, kinawaalika wanachama wake wote, wakereketwa na wananchi kwa ujumla kuhudhuria katika mkutano huo mkubwa. Mkutano utafanyika kwa amani na utulivu na wote mnakaribishwa.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Imetolewa na:
JUMA SIMBA
KATIBU WA SIASA NA UENEZI
MKOA WA DAR ES SALAAM.
07/06/2012

JAMAA WAKUTANA NA ADHA YA WANAJESHI ALMAARUFU KAMA WAJEDA.

Kila siku mnaambiwa msipite maeneo yao hawa jamaa lakini raia hamkomi.
wanajeshi walivyo msuba.............inaweza ndio ikawa shughuli ya siku nzima.........mkacheza kiduku hapooo hadi maji yatakapokauka............hawana tatizo na mtu, watapeana zamu ya kwenda kula ila raia ndio mtakausha huo Mto. 

KCB TANZANIA YAZINDUA HUDUMA MPYA YA DISPORA BANKING

Mwenyekiti Mtendaji wa Benki ya KCB Tanzania DK Edmund Mndolwa akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma ya KCB DIASPORA BANKING uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti Mtendaji wa Benki ya KCB Tanzania Dk Edmund Mndolwa, akizindua rasmi huduma mpya inayotolewa na KCB DIASPORA BANKING, Katikati ni Mmoja wa Mameneja wa benki hiyo SHOSE KOMBE. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo MOEZ MIR.

Baadhi ya Wafanyakazi wa Benki ya KCB Tanzania wakifuatilia kwa makini uzinduzi wa huduma mpya ya KCB DIASPORA BANKING iliyoanzishwa na benki hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya KCB Tanzania Christine Manyenye akifafanua kuhusiana na huduma mpya iliyoanzishwa na benki hiyo ya KCB DIASPORA BANKING wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Wafanyakazi wa Benki ya KCB Tanzania wakifuatilia kwa makini uzinduzi wa huduma mpya ya KCB DIASPORA BANKING iliyoanzishwa na benki hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam

Sakata la Mafuta Jijini Mbeya: Mafuta ya Taa Jijini Mbeya ya panda bei kutoka Tsh 2175 mpaka kufikia Tsh 3000 na 3500. Ni Kutokana na uhaba wa Mafuta hayo.

Wananchi wa Jiji la Mbeya wakiwa wana haha kupata Mafuta ya taa katika kituo cha mafuta
Baadhi ya Njinga zikiwa zimepaki eneo ambalo ndilo pekee Mafuta yanapatikana jinini Mbeya
Mdau akiwa anatazama vema kama anazo pesa za kununua Mafuta hayo baada ya kushtuka kuambiwa kuwa bei imepanda mpaka kufikia 3500
Kila mtu anataka kupata mafuta kwa muda katika eneo hilo Mpaka wenye mapipa nao wamo.

KITUKO KUTOKA KWENYE AKAUNTI YA FACE BOOK YA JOHN KITIME LEO!

Mwanamuziki nguli John Kitime
Joji alikuwa shule ya vidudu na akaanza kujua hesabu. Mjomba wake akaja;
JOJI: Mjomba najua hesabu.
MJOMBA: Tatu kujumlisha mbili?..Mtoto akaanza kuhesabu vidole akamaliza;
JOJI: Tano
MJOMBA: Haya sasa sitaki uhesabu vidole. Tia mikono yako kwenye mifuko ya kaptura. Haya tano kujumlisha tano?....mtoto akaanza kuhesabu vidole mfukoni.
JOJI: Kumi na moja!!
Haaaa haaaa haaaa haaaaa!!!! Joji you are Very Bright!

KAMATI ZA BUNGE ZAENDELEA NA KAZI YA KUPOKEA MAKADIRIO YA BAJETI ZA WIZARA LEO


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufunzo Mhe. Shukuru Kawambwa akiwasilisha makadirio ya bajeti ya Wizara yake mbele ya Kamati ya Huduma za Jamii kabla ya kupelekwa Bungeni. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Mhe. Magareth Sitta na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Faustine Ndugulile.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Huduma za Jamii Mhe. Faustine Ndugulile (kushoto) na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Magareth Sitta (katikati) wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufunzo Mhe. Shukuru Kawambwa alipokuwa akiwasilisha makadirio ya bajeti ya Wizara yake mbele ya kamati hiyo leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii Mhe. Jenister Mhagama akisisitiza jambo wakati wakipokea makadirio ya bajeti ya wizara ya kazi na Ajira iliyo wasilishwa mbele ya kamati hiyo. Kushoto kwake ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Juma Nkamia na Kulia ni Katibu wa Kamati hiyo Chacha Nyakega, Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudensia Kabaka na naibu waziri wa Wizara ya kazi na Ajira Mhe. Dkt Milton Makongoro Mahanga.
Mwenyekiti wa Kamati ya fedha na Uchumi Mhe. Andrew Chenge akifafanua jambo mbele ya wajumbe wakamati na watendaji kutoka wizara ya fedha baada ya kupokea mapendekezo ya bajeti ya wizara ya fedha yaliyo wasilishwa mbele ya kamati hiyo leo. Kulia kwake ni Waziri wa fedha Mhe. William Mgimwa Mhe Saada Mkuya Salum na Mhe Janet Mbene, amabo ni Manaibu waziri katika wizara hiyo.
Mjumbe wa kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma Mhe.Murtaza Ally Mangungu akifurahia jambo baada ya kupokea hesabu zilizokaguliwa za chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kwa mwaka 2010/2011. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. zitto Kabwe na Kushoto ni Katibu wa Kamati hiyo Erick Maseke
kamati ya POAC ikiendelea na kazi.
Picha zote na Owen Mwandumbya wa Bunge

AUWA NA KISHA KUNYOFOLEWA UUME, NA MIKONO MKOANI ARUSHA


KAMANDA WA POLISI WA MKOA WA ARUSHA LIBERATUS SABAS
(NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA)
Mtu mmoja ambaye hajajulikanan jina lake amefarikidunia huku baadhi ya viungo vyake hasa sehemu za uume wake zikiwa zimechomolewa pamoja na mikono yake
Akiongea na waandishi wa habari mapema leo kamanda wa polisi mkoa wa arusha Sabas Liberatus alisema kuwa tukio hilo lilitokea may 26 majira ya saa tni asubuhi katika eneo la Mto Nambala wilyani Arumeru
Kamanda Sabas alisema kuwa katika siku ya tukio mytu mmoja mwenye jinsia ya kiume ambaye hajatambulika mpaka sasa anakadiriwa kuwa na miaka25-30 alikutwa akiwa amefariki
Kamanda huyo aliongeza kuwa mara baada ya wapita njia kumkuta akiwa amefariki waligundua kuwa pia hana viungo mbalimbali ndani ya mwili wake hali ambayo ilizua tafrani kubwa
‘hawa watu walipomuangalia kwa undani sana waliweza kujua na kutambua kuwa baadhi ya viungo vyake havipo na ndipo walipota taarifa kwa jeshi la polisi na sisi tulipoofika ndani ya eneo la tukio tuliyakuta hayo hayo”alisema Kamanda Sabas
Pia aliongeza kuwa baada ya polisi kufika katika eneo la tukio walikuwa mwili huo ukiwa na suruali aina ya jeans ambayo ilikuwa imeshushwa hadi chini ya magoti na viungo vyake vikiwa vimenyofolewa
Hataivyo jeshi hilolinaendela na upelelezi juu ya tukio hilona upelelzi wa kumfahamu chanzo cha umati huo huku mwili wa marehemu ukiwa umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mount Meru

Waziri akizungumza na Kamati ya Bunge

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Terezya Huvisa akizungumza na Kamati ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Mazingira kwenye ukumbi wa Hazina kulia Mwenyekiti wa Kamati hiuo James Lembeli kushoto Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga,Naibu katibu Mkuu Eng Ngosi Mwihava,Mh Zakhia Megji kikao hicho kimefanyika leo Mjini Dar es Salaam[Picha na Ali Meja

Baraza la Sanaa (BASATA) lawapa somo waandaaji wa Epic Bongo Star Search 2012





Na Mwandishi Wetu

BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limeendesha semina ya siku moja kwa majaji wa shindano la Epic Bongo Star Search 2012 kwa kuwataka kuzingatia maadili ya kazi zao.

Akitoa somo kwa majaji hao mratibu wa matukio wa Basata Malimi Mashili aliwataka majaji hao kutambua kuwa asilimia kubwa ya washiriki wanategemea zaidi msaada wao katika kukuza vipaji.

Mashili aliwataka majaji hao kutambua kuwa mazingira waliyotoka washiriki na kuangalia namna ya kuwasaidia kulingana na mikoa yao kwa kuwa wapo ambao wana vipaji lakini wanatatizwa na suala la kuyazoea mazingira.

Alisema kuwa kwa kuwa mwaka huu EBSS itaruhusu washiriki wa miaka 16 hivyo ni vema zaidi wakazingatia suala la sauti kulingana na umri wa mshiriki sababu watakuwepo wenye sauti za kitoto pia.


Pia aliwataka majaji hao kuhakikisha kuwa hawatoi aina yoyote ya upendeleo na wala kuwa karibu zaidi na baadhi ya washiriki wa shindano hilo.

Pia alisisitiza kuwa majaji wanalo jukumu kubwa la kuwaelekeza namna ya kuimba, kuvaa, kujiheshimu na usafi wa mwili pia.

“Hiii ni semina ya kuwekana sawa tu kwa kuwa hili shindano lipo kwa muda mrefu na majaji mmekuwa mkifanya vema, kwa niaba ya BASATA napenda kuchukua muda huu kuwataka muwe makini katika kuzingatia maadili haya niliyoyasema na hata mengine pia”alisema Mashili.Naye Mkurugenzi wa Berchmark Production inayoandaa shindano hilo Ritha Paulsen alisema kuwa semina hiyo ni muhimu kwa majaji kwa kuwa muda mzuri wa kukumbushana mambo muhimu yahusuyo muziki.

Epiq Bongo Star Search mwaka huu inaanzia mkoani Dodoma Juni 16 katika ukumbi wa Royal Village.

Majaji wa shindano hilo waliohudhuria ni pamoja na Jaji Mkuu Ritha Paulsen, Master Jay, Salama pamoja na mratibu wa EBSS kutoka Basata Vicky Temu.


MWENYEKITI WA KLABU YA SIMBA ASEMA: MKATABA WA YONDAN YANGA NI BATILI


Simba Sports club imesikitishwa na kitendo cha Young Africans kuvunja taratibu za usajili kwa kumrubuni mchezaji wake Kelvin Patric Yondani kwa kuzungumza naye na baadae kwa ushahidi wa picha kuonekana wakimuandikisha makaratasi ambayo baadae imeripotiwa na vyombo vya Habari kwamba alikuwa akisaini mkataba wa kuichezea timu hiyo ya Young Africans.
Kwamba katika picha hiyo ameonekana mjumbe wa Young aliyejiuzuru bwana Seif Ahmed na hilo lilitoa shaka kama utaratibu huo umefanywa na klabu ya Young, lakini shaka hiyo imeondolewa pale ambapo tovuti ya Young imetangaza kumsajili mchezaji huyo wa Simba SC, lakini zaidi ya hilo picha inaonyesha fedha zikiwa zimewekwa mbele ya mchezaji jambo linaloonyesha mazingira ya kurubuniwa kwani kwa utaratibu wa kifedha, pesa nyingi kiasi hicho malipo yake yanashauriwa/yanapashwa kupitia benki.
Mbali ya hayo picha hiyo inamuonyesha Kelvin akiwa katika jezi ya mazoezi ya timu ya Taifa na yenye logo ya Kilimanjaro na kumbukumbu zinaonyesha mkataba kati ya TBL na TFF tarehe 9/5/2012, kwa haraka haraka tukio hilo limefanyika katika kipindi chini ya mwezi mmoja ingawa taarifa za ushahidi zinaonyesha tukio hilo limetokea jana tarehe 6/6/2012.
Simba Sports Club ilipenda kuamini kwamba tukio hilo haliihusu klabu ya Young kwani bwana Seif Ahmed alishajiuzuru kutoka kwenye kamati ya Young Africans, kwani Young ni klabu kongwe na inayojua taratibu zote za usajili.
Kwamba Simba Sports Club imeshawasiliana na jopo lake la mawakili na inajiandaa kuishtaki klabu ya Young katika chombo husika cha mpira na kudai adhabu ya kutopitisha majina yote ya usajili ya Young kwa mwaka 2012/2013 na miaka mingine miwili ijayo na Simba SC ipo tiyari kufuatilia suala hili hadi katika mahakama ya mpira ya FIFA.
Kelvin Yondani ni mchezaji halali wa Simba Sc aliye na mkataba hadi 31 mei 2014 mkataba ulioongezwa tarehe 23/12/2011 kuundeleza mkataba wa awali uliokuwa unaisha tarehe 31/5/2012. Sheria za FIFA za hadhi na uhamisho wa wachezaji ziko wazi katika kipengele cha 5 kifungu kidogo cha 2 kinasema kwamba mchezaji atasajiliwa kuichezea timu moja tu kwa wakati mmoja.
Imetolewa   tarehe 7/6/2012.
MH. ISMAIL ADEN RAGE (MB)
MWENYEKITI
SIMBA SPORTS CLUB

Rais Dk. Shein akutana na Balozi wa Msumbiji na Sweden


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali
Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania Amour
Zakaria aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais,kwa kumaliza muda
wake wa kazi nchini.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali
Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania Amour
Zakaria aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais,kwa kumaliza muda
wake wa kazi nchini.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Sweden Nchini
Tanzania Lennarth Hjelmaker,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar
kujitambulisha kwa Rais.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini
Tanzania Lennarth Hjelmaker,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar
kujitambulisha kwa Rais.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

RAIS KIKWETE AAGANA NA BALOZI WA CANADA


Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete leo Juni 7, 2012 katika Ikulu ya Dar es salaam
amekutana na kuagana na Bw Robert J. Orr, Balozi wa Canada nchini, anayemaliza muda wake wa uwakilishi.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Bw Robert J. Orr, Balozi wa Canada nchini, anayemaliza muda wake wa uwakilishi.

GAMBIA KUWASILI LEO USIKU TAYARI KWA MPAMBANO WAO NA TAIFA STARS



Timu ya Taifa ya Gambia (The Scorpions) ambayo awali ilikuwa iwasili nchini leo (Juni 7 mwaka huu) saa 1.40 asubuhi sasa itawasili leo saa 9.20 usiku kwa ndege ya Kenya Airways tayari kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa Stars.
The Scorpions ilipaswa kubadili ndege Dakar, Senegal jana usiku lakini kukawa na ucheleweshaji (delay), hivyo ikashindwa kuwahi Nairobi, Kenya ambapo ingeunganisha kwa ndege ya alfajiri kuja Dar es Salaam.
Kikosi cha timu hiyo chenye wachezaji 22 wakiwemo tisa wanaocheza mpira wa kulipwa nje ya nchi hiyo kitafikia kwenye hoteli Sapphire iliyopo Mtaa wa Lindi na Sikukuu eneo la Kariakoo.
Wachezaji walioko katika msafara huo ni Musa Camara, Abdou Jammeh, Momodou Futty Danso, Lamin Basmen Samateh, Ousman Koli, Pa Saikou Kujabi, Mustapha Kebba Jarju, Yankuba Mal Ceesay na Demba Savage.
Wengine ni Saihou Gassama, Alieu Darboe, Momodou Ceesay, Pa Modou Jagne, Tijan Jaiteh, Bubacarr Sanyang, Christopher Allen, Musa Yaffa, Sulayman Marr, Mamut Saine, Hamsa Barry, Ali Sowe, Omar Colley na Saloum Faal.
PROGRAMU YA MAZOEZI YA GAMBIA
IJUMAA JUNI 8
01.00 asubuhi Mazoezi- Uwanja wa Karume
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa
JUMAMOSI JUNI 9
04.00 asubuhi Mkutano na Waandishi wa Habari- Ukumbi wa TFF
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti Wa CUF Profesa ibrahim Lipumba Wahudhuria Mazishi Ya Mwenyekiti Mstaafu Wa CUF Marehemu Musobi Mageni

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akitoa salaam za pole kwa viongozi na chama cha Wananchi CUF na wananchi wa mkoa wa Mwanza katika mazishi ya Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, marehemu Musobi Mageni
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akiweka udongo kwenye kaburi la Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, marehemu Musobi Mageni ,kulia kwake ni Mwenyekiti wa Cuf Profesa ibrahim Lipumba ambao wote walijumuika na viongozi na chama cha Wananchi CUF na wananchi wa mkoa wa Mwanza katika mazishi ya Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, marehemu Musobi Mageni
--
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amejumuika na viongozi wa chama cha Wananchi CUF na wananchi wa mkoa wa Mwanza katika mazishi ya Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, marehemu Musobi Mageni huko kijijini kwao Ngudu, Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Katika mazishi hayo, pia alihudhuria Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, Makamu Mwenyekiti, Machano Khamis Ali, pamoja na wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa, wakiwemo Waziri wa Afya Zanzibar, Juma Duni Haji na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Haki za Binaadamu, Salum Bimani.
Marehemu Musobi alifariki Dunia Mei 30, mwaka huu nyumbani kwake Ngudu baada ya kusumbuliwa na maradhi ya shinikizo na damu na sukari kwa muda mrefu.
Marehemu alihamia chama cha Wananchi CUF mwaka 1994 na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Taifa mwaka 1995 hadi 1999 alipostaafu na kubaki kuwa Mjumbe wa kudumu wa Baraza Kuu la Taifa na Mkutano Mkuu wa chama hicho hadi kifo chake.
Katika uhai wake, marehemu aliwahi kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mijini kuanzia mwaka 1972 hadi 1975, mwaka 1976 hadi 1978 Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala Rajan Industries Ltd. Nafasi nyengine ni alizowahi kushikilia ni Ubunge na Mkuu wa Wilaya katika wilaya ya Chunya, Kahama na Muleba.
Akitoa salamu za rambirambi, Makamu wa Kwanza wa Rais, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad wakati wa mazishi alisema, marehemu alikuwa kisima cha busara na mwenye hekima kubwa na ndio maana viongozi wa CUF walikuwa wakikimbilia kwake kuchota ushauri wake.
“Huu ni msiba mkubwa sio tu kwa familia yake, bali kwa chama chetu na kwa serikali zote mbili”, alisema Maalim Seif.
Marehemu ambaye alizaliwa mwaka 1930, ameacha wajane wawili, watoto 15, wajukuu 28 na vitukuu sita.
Na
Khamis Haji
Ofisi Ya Makamu wa Kwanza Wa Rais Zanzibar

MILIONI 421.8 ZAPATIKANA KUCHANGIA MPANGO WA ELIMU KATA YA KIPAWA JIJINI DAR ES SALAAM

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Dk. Makongoro Mahanga (kulia), Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto) na Mwenyeji wa harambee ya kuchangia mpango wa elimu wa Kata ya Kipawa, Diwani wa Kata hiyo Bonah Kaluwa, wakimuongoza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ambaye alikuwa mgeni rasmi kuingia ukumbini Katika hafla iliyofanyika jana usiku ndani ya hoteli ya Kilimanjaro (Kempiski hotel) jijini Dar es Salaam .
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye harambee hiyo
Diwani wa Kata ya Kipawa Bonah Kaluwa, akitoa neno la shukurani kabla ya kuanza kwa harambee hiyo.
Mgeni rasmi wa Hharambee hiyo akimpa mkono wa asante mwakilishi wa kampuni ya Home Shopping Centre Bi Madiha Al Harthy (kushoto),Salma baada ya kuchangia sh. milioni 22.
Mkurugenzi wa SONGAS Limited Bw;Christopher Ford(katikati),akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya dolla za kimarekani 10,000, mgeni rasmi wa harambee hiyo.kushoto meneja
rasilimali Songas Bi Agatha Keenja.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja (katikati) akipongezwa na Mgeni rasmi wa harambe hiyo baada ya kuchangia sh. 500,000.

eya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto), akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh.milioni 10, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia mpango wa elimu Kata ya Kipawa, iliyofanyika Dar es Salaam juzi. Fedha hizo zilitolewa na Manispaa hiyo ambapo zaidi ya sh. milioni 400 zilipatikana.
Na Dotto Mwaibale
WAZIRI Mkuu wa zamani , Edward Lowassa, ameendeleza kuwa mstari wa mbele katika harakati zake za kuchangisha mamilioni ya fedha baada ya kuchangisha Sh.421,850,000 kwa ajili ya kuboresha Mfuko wa Elimu Kata ya Kipawa katika Manispaa ya Ilala Jijini Dar es Salaam.
Lowassa ambaye ni mbunge wa Monduli (CCM), aliendesha harambee hiyo juzi katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Kempiski Jijini Dar es Salaam ambapo yeye mwenyewe alichangia Sh.milioni 10.
Katika harambee hiyo miongoni mwa makampuni yaliyochangia kiasi kikubwa ni Lion Club Sh.milioni 70, Home Shipping Center Sh.milioni 22, African Barrick Gold Dola 10,000, Songas Dola 10,000, Maersk Sea Line ilichangia Sh.Miliono 90, na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja alichangia milioni Sh.10.
Wengine waliochangia ni madiwani, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, Chadema, taasisi za watu binafsi na mtu mmoja mmoja ambapo Radio Clauds walitoa muda wa hewani wa kutangaza mpango huo wenye thamani ya sh. milioni 12.
Akizungumza kabla ya kuendesha harambee ya kuchangisha, aliwataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kuwahamasisha wananchi kuwekeza katika kuchangia sekta ya elimu.
Lowassa alimpongea Diwani wa Kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa, kwa jitihada zake alizozionyesha za kuchangia elimu na kuwataka madiwani wengine kuiga mfano huo.
Diwani wa Kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa, kwaupande wake alisema shule saba za Msingi na Sekondari zilizopo kata hiyo zinakabiliwa na matatizo lukuki ikiwemo upungufu wa vyumba vya madarasa hali inayosababisha wanafunzi kati ya 140 hadi 160 kusomea katika darasa moja.

“Shule za kata yangu kwa kweli zinakabiliwa na changamoto nyingi, kwa mfano Shule ya Msingi ya Majani ya Chai ina vyumba vya madarasa nane wakati wanafunzi waliopo ni 2,200, Shule ya Msingi ya Minazi Mirefu madarasa yake yaliyopo ni machakavu pia hayatoshelezi,”alisema Kaluwa.
Kaluwa alisema jitihada nyingine zilizofanywa katika kutafuta pesa kwa ajili ya kuziboresha shule hizo ambapo Machi 17 mwaka huu kuliitishwa matembezi ya hisani yaliyoongozwa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
Aliongeza kuwa katika hafla hiyo kiasi cha shilingi milioni 15 kilichangwa na wadau mbalimbali ambapo kati ya hizo Sh.Milioni 3 zilitolewa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Clouds Media Group ambao walitoa shilingi milioni moja na wanafunzi kadhaa wa shule za msingi na sekondari.
Mbunge wa Jimbo la Segerea Dk.Makongoro Mahanga aliwashukuru wadau waliojitokeza kuchangia kata hiyo ambayo ipo katika jimbo lake na kuwataka wadau wengeni kuchangia kata zingine ili kukabiliana na matatizo hayo katika shule mbalimbali

Tawi la CHADEMA Washington DC Nchini Marekani Lazidi Kuvuna Wanachama Wapya

Linda Bezuidenhout (LB) furaha baada ya kuvua kamba kuvaa kwanda na kuchukua kadi kuwa mwanachama kamili wa Chama Cha Demokrasia Chadema.
Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe. Kalley Pandukizi, pamoja na katibu wake Mhe. Libe Mwang'ombe akimkabidhi rasmi mwanacham mkareketwa ambae ni mwana mitindo Linda Bezuidenhout (LB) kati ya uwanachama wa chama cha Demokrasia Chadema katika ofisi ya tawi la Tawi la Chama Washington DC.
Mwenyeketi wa Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Kalley Pandukizi akiwa na katibu wachama hicho,Ndugu Libe Mwang'ombe alipotoa kadi rasmi kwa Beautician maharufu na designer wa kitanzan Linda Bezuidenhout (LB)
Viongozi wa tawi la chadema Washington DC wakipata Champagne
Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe. Kalley pamoja na katibu wake Mhe. Libe Mwang'ombe wakipata picha ya pamoja na Linda Bezuidenhout Atlanta, Georgia na wanachama wa tawi la chadema Washington DC.
Katika miaka ya nyuma Linda aliwahi kusponsor matukio mbali mbali kwenye miaka ya 1990 wengi wao wakimjua kwa Linda Express Nchini Tanzania ambae ambaye hivisasa anajishughulisha na biashara ya nguo za kiume milanovita.com pamoja na zakike ambazo anadesign mwenyewe kwa brand name ya Linda kutoka Atlanta, Georgia Nchini Marekani.Picha na Mdau Wa Swahilivilla

TANGAZO LA OFISI YA MKUU WA MKOA WA RUKWA :UPOTEVU WA VITABU ISHIRINI (20) VYA LESENI YA BIASHARA


Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa inapenda kuutangazia Umma kuwa imepotelewa na vitabu ishirini (20) vya leseni za biashara vilivyopotea tarehe 22 Mei 2012 katika moja ya Daladala Jijini Dar es Salaam.
Vitabu hivyo vilivyotolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara vikiwa na kumbukumbu namba 1389501 mpaka 1391500.
Kwa yeyote atakayeona vitabu hivyo au kuvinunua anaombwa avipeleke kituo chochote cha polisi kilicho karibu yake au kutoa taarifa juu ya mwenye navyo katika kituo hicho.
Ifahamike kuwa vitabu hivyo ni batili hivyo haviruhusiwi kutumika kwa namna yeyote ile. Na atakayethibitika kuvitumia atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zilizowekwa.
Ewe mfanyabiashara, epuka manunuzi na matumizi ya vitabu vyenye namba tajwa hapo juu kwa usalama wa biashara yako.
Kwa mawasiliano tunaomba mtumie namba zetu hapo juu.
Tunaomba ushirikiano wenu.
IMETOLEWA NA
HAMZA TEMBA
AFISA HABARI MKOA WA RUKWA
07/06/2012

YONDAN AKIMWAGA WINO YANGA NA KITITA CHAKE CHA MIL.30

KELVIN Patrick Yondan, beki wa kati wa Simba amekana kusaini mkataba wowote na Simba na amesema yeye amesaini Yanga tu mkataba wa miaka miwili.
Yondan amesema Simba wanampakazia kusaini mkataba mpya na anataka wapenzi wote wa soka Tanzania watambue kwamba kuanzia sasa yeye ni mchezaji halali wa Yanga.
Yondan aliikana Yanga awali kwa sababu walimsainisha fomu bila kumpa fedha, lakini leo amepewa Milioni 30 zake taslimu na amemaliza kila kitu.

TIKA itaboresha huduma Ilala- Meya wa Ilala Jerry Slaa

Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Slaa akufungua semina ya Mpango wa bima ya Afya unaojulikana kama TIKA uliobuniwa na Mfuko wa Bima wa Afya (NHIF) inayotolewa kwa madiwani wa Manispaa hiyo inayofanyika kwenye ukumbi wa Arnautoglo Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam asubuhi hii, kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa NHIF Bw Khamis Mdee na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Ellias Mwasabwite.
Naibu Mkurugenzi wa NHIF Bw Khamis Mdeeakizungumza katika semina hiyo kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Ellioth Mwasabwite na katikati ni Meya wa Ilala Mh. Jerry Slaa.
Wakurugenzi na maafisa kutoka Mfuko wa Bima wa Afya wakiwa katika semina hiyo leo.
Madwani wanaoshiriki katika semina hiyo wakifuatilia kwa makini mada katika semina hiyo.
Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Slaa kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa NHIF Bw. Khamis Mdee na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Ellias Mwasabwite.
Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Slaa kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa NHIF Bw. Khamis Mdee na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Ellias Mwasabwite.